YC-Dialogue
 
 
Karibu kwenye Tovuti yetu  
The unicef  Infomation Resouce Centre,Dar es salaam Tanzania......

Ripoti za Midahalo    

Sign up, Members Sign in  .

Chat na mtu Online  

Habari mpya Wasiliana nasi  Tovoti mbalimbali  Picha mbalimbali  Kitabu cha Wageni

Go to home page

 

 

Youth Dialogues @Unicef Conference hall
    Youth Dialogue History
 
 

MDAHALO WA VIJANA NI NINI ?

Ni uwanja pekee unaotupa fursa Vijana na Watoto wa Tanzania kukaa pamoja ili kujadili mambo muhimu ya kijamii yanayo tugusa .Hii ni pamoja na kujaribu kutafuta suluhisho la Baadhi ya matatizo yanayoikumba Jamii ,Hususani Vijana na Watoto.

Baadhi ya matatizo ya Kiuchumi na Kijamii yanayo jadiliwa ni pamoja na ,Suala zima la Umasikini ,Mazingira Magongwa hususani Gongwa hatari la Ukimwi,Siasa ,Haki za Binaadamu,Elimu na Masuala yote yanayo mtatiza Mwananchi.

 

HISTORIA FUPI.

Mdahalo huu ulianza mnamo miaka miwili iliyopita ,Chanzo kikiwa ni Mawazo ya Wanafunzi wa Mkoa wa Dar es salaam ,Kukaa pamoja ili kutafuta mbinu za kuchangia katika maendeleo ya jamii yetu kwa njia moja au Nyingine .

Baada ya muda mfupi tuliokuwa Wanafunzi tuligundua kuwa tutakuwa hatujawatendea haki Vijana walioko nje ya shule ,Hivyo Tuliamua kutafuta sehemu ambayo itaweza kutunufaisha vijana wote bila kujali tunakotoka ili mradi kwa Dhumuni moja la Ujenzi wa Taifa .

Wazo letu lilipokelewa kwa mikono miwili na shilika la Kimataifa la Kuudumia Watoto (UNICEF).Hawa walitupa nafasi ya kuutumia Ukumbi wao wa mikutano kila Jumamosi ya Kwanza ya Mwezi.Baada ya kuzigundua Juhudi zetu,Sasa UNICEF wanatusaidia katika masuala mbalimbali,mfano,Gharama zote za Uendeshaji.

 

DHUMUNI.

Dhumuni kuu ni kuwaweka Vijana na watoto pamoja ili waweze kufanya maamuzi ya maendeleo ya Jamii yao kwa sauti moja.Kwa kuzingatia Takwimu zilizopo,tuliono Vijana na Watoto ndio wengi katika Jumla ya watu Hapa Tanzania,Hivyo maamuzi ya busara kutoka kwa Vijana na Watoto ni mchango mkubwa wa maendeleo ya Taifa letu.

Vijana tunaizingatia Methali ya Kichina isemayo kuwa ,``Kama watu elfu moja watapiga risasi wakilenga shabaha moja tu na kwa wakati mmoja,huna sehemu ya shabaha ambayo haitapigwa’’.

Hivyo wachache tuliona ni Busara tuwahamasishe Vijana wenzetu ili tuwe wengi,kusudi tunapolenga shabaha kwa wakati mmoja ,isibaki sehemu isiyopigwa.

Pia tumezingatia wito wa Rais wetu,Mheshimiwa Benjamin Mkapa ,unaotaka mipango yote ya maendeleo itokane na wananchi wenyewe badala ya kutoka Serikali Kuu.Hivyo tunaiona ni fursa muhimu kwetu kama Vijana kuweza kutoa mchango wetu katika maendeleo (Shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais)

Pamoja na hilo Mdahalo wa Vijana una dhumuni kubwa la kuhamasisha maendeleo ya Vijana kupitia njia mbalimbali kama ifuatavyo;-

(a)Kuiunganisha Serikali na mashilika yasiyo ya Kiserikali(Non-Gorvernment Organizations),Mashilika ya kimataifa ,Vyombo vya habari na Jamii kwa Ujumla ili kuongeza uelewa juu ya mambo yanayo wahusu Vijana ,Mathalani dawa za kulevya, magonjwa,Ajira na mengine mengi.

(b)Kuanzisha malengo endelevu yanayodhamilia kuwaendeleza na kuwashilikisha Vijana wa jinsia zote

katika maendeleo ya taifa.

(c )Kuufanya Mdahalo wa vijana uwe nafasi ya Vijana kujifunza mambo mbalimbali ya Jamii,mfano Haki za uchaguzi,Wajibu na haki za Binadamu na mengine kama hayo .

(d)Kuwashauri Vijana,waweze kutumia maliasili tulizonazo nchini ili kutatua matatizo yetu ya Kijamii na kiuchumi.

(e)Kuishauri Serikali katika masuala yote yanayowahusu Vijana,hususani Haki na Wajibu wa Vijana katika jamii.

(f)Kuwaunganisha Vijana wote wa Tanzania kwa malengo ya kuvumbua na kuendeleza Vipaji vyao.

 

MIKAKATI ILIYOPO.

(1)Kuakikisha malengo /madhumuni ya mdahalo huu wa Vijana yanafikiwa na Vijana wenyewe kwa faida yao na jamii kwa ujumla.

(2)Tuna mpango wa kuanzisha ushirikiano wa Vijana wa Nchi za Afrika Mashariki na baadae Afrika ya Kati ili Kubadilishana uzoefu katika utatuzi wa matatizo yanayo wakabili Vijana,hususani suala zima la ugonjwa wa Ukimwi ,Vita na Madawa ya kulevya.

(3)Tunao mpango wa kuishawishi Serikali pamoja na mashilika ya kimataifa kutusaidia kuitisha mkutano wa Vijana wa Afrika mashariki na Kati ili tutumie nafasi hiyo Kuongelea suala la Vita.Lengo kuu likiwa ni kuwashawishi na kuwashauri Vijana Wenzetu wa nchi zenye Vita kama vile,Rwanda ,Burundi,Jamuhuri ya watu wa Congo na Uganda,wasikubali kushilikishwa katika vita ili njia hiyo isaidie kupunguza vita katika Nchi zao.

Mkakati huo bado tuna ujadili kwani ni mkakati wa gharama.Lakini tuna mpango wa kuwaomba UNICEF na Mashilika mengine ya kimataifa yanayo hudumia nchi zenye Vita,Kutusaidia kwa hali na mali kufikia lengo letu .

(4)Tunao mgo wa kuiomba serikali nafasi ya kuwa tunashiriki katika mikutano mikuu, hasa linapokuja suala la kuwakeana mikataba ya Amani kwa Nchi zenye matatizo ya Vita,ili nasi tuweze kutoa ushawishi na kilio chetu kwa hao wanao ng’ang’ania vita,ili waone ni kwa kiasi gani Vita inawaumiza na Kuwaathili kwa kiasi kikubwa Vijana wenzetu katika nchi hizo.

MAFANIKIO.

/1/ Kama Vijana, tumeweza kushiriki katika maamuzi mbalimbali ya Taifa, Kwa mfano,Tulishiriki vema katika urekebishaji wa Sera ya vijana ,tunaishukuru Wizara ya kazi , Michezo na maendeleo ya Vijana kwa kutushirikisha katika maamuzi hayo.

/2/ Vijana wenzetu wachache walifanikiwa kupeleka ripoti juu ya Umasikini katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee wakati wa wiki ya sera ya umasikini (Poverty Policy Week).

/3/ Tumefanikiwa kuwaunganisha Vijana kwa asilimia zipatazo 55% ,Kwani kupitia katika Tovuti (Website) www.youthdialogue.gobot.com ,tuliyo ianzisha, Vijana kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania wameweza kujua lengo letu na sasa wanatoa maoni yao .Tovuti hiyo ni changa moto kwa vijana wote nasasa tuko katika mkakati wa kuitangaza ili na wenzetu kutoka Nje ya Tanzania waweze kuungana nasi.

/4/ Ushirikiano kati ya Vijana na Watoto umekuwa madhubuti kwani wamefikia kuwa na uwezo wa kuendesha vipindi vyao katika Radio na T.V, hali ambayo imewapatia fursa ya kuzijua haki zao nawajibu wao miongoni mwa jamii.

/5/ Tumekuwa mstari wa mbele kutoa ujumbe na kujadili mambo mbalimbali katika siku maalumu kupitia vyombo vya Habari mfono,Siku ya Mtoto wa Africa,siku ya Ukimwi duniani,Wiki ya umasikini na nyinginezo .

/6/ Kikubwa tumefanikiwa kufanya mdahalo huu uwe uwanja wa mafunzo kwa Vijana wenzetu,kwani kwa kipindi hiki kifupi wote tume elimishwa mambo mbalimbali kama ifuatavyo ,

(a).Rushwa [Afisa kutoka kitengo cha kuzuia Rushwa ]

(b).Utandawazi na mawasiliano

(c). Uwakilishi wa kijana bungeni [Mheshimiwa Lazaro Nyalandu MP]

(d).Tanzania bila umasikini .

(e)Uboreshwaji wa Sera ya Vijana ya mwaka 1996

Mwisho tunatoa shukrani za dhati kwa wote wanaoshirikiana nasi katika kulisukuma Gurudumu la Maendeleo.Shukrani za pekee ziwaendee serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutushilikisha kama njia moja wapo ya kutuwezesha.UNICEF ni ndugu zetu wa damu ambao vijana wote kwa Sauti moja,tunamuomba Mungu awasaidie ili nasi tuweze kufikia Malengo yetu.

Mungu Ibariki Tanzania Mungu ibariki Afrika.

 

Waandaji;-

FRANK RICHARD

ARNOLD KAYANDA

ATHANAS WILLIAM


 

                                                                                 

                                                        Go to home page

r


 

                                         Youth Dialogue (c)2004